a Kut 20:23; Amu 17:3-4; Isa 30:22; Kum 9:16; Neh 9:18; Za 106:19; Mdo 7:41; Kut 20:23; Isa 42:17; 1Fal 12:28; 14:9; 2Fal 10:29; 17:16; 2Nya 13:8; Hos 8:6; 10:5
Exodus 32:4-9
4 aAkavichukua vile vitu walivyomkabidhi, akavifanyiza kwa kusubu sanamu yenye umbo la ndama, akaichonga kwa kutumia chombo. Kisha wakasema, “Hii ndiyo miungu yenu, ee Israeli, iliyowapandisha kutoka Misri.” 5 bHaruni alipoona hili, akajenga madhabahu mbele ya yule ndama na kutangaza, “Kesho kutakuwa na sikukuu kwa Bwana.” 6 cKwa hiyo siku iliyofuata watu wakaamka asubuhi na mapema na kutoa sadaka za kuteketeza na sadaka za amani. Baadaye watu wakaketi kula na kunywa, nao wakasimama, wakajizamisha katika sherehe. 7 dKisha Bwana akamwambia Musa, “Shuka, kwa sababu watu wako, uliowatoa Misri, wamepotoka. 8 eWamekuwa wepesi kugeuka na kuacha niliyowaamuru, na wamejitengenezea sanamu ya kuyeyusha yenye umbo la ndama. Wameisujudia na kuitolea dhabihu, nao wamesema, ‘Hii ndiyo miungu yenu, ee Israeli iliyokupandisha kutoka Misri.’ ” 9 f Bwana akamwambia Musa, “Nimeona watu hawa, nao ni watu wenye shingo ngumu.
Copyright information for
SwhKC